SDF SPORTS SDF SPORTS Author
Title: NDANDA: TUNAHITAJI POINTI TATU ZAIDI YA SIMBA
Author: SDF SPORTS
Rating 5 of 5 Des:
Ndanda FC imesisitiza kuwa inahitaji zaidi pointi tatu kwenye mchezo wa kesho dhidi ya Simba kuliko Wekundu hao kutokana na kuwa kwenye ha...
Ndanda FC imesisitiza kuwa inahitaji zaidi pointi tatu kwenye mchezo wa kesho dhidi ya Simba kuliko Wekundu hao kutokana na kuwa kwenye hali mbaya ya kushuka daraja.

Ndanda ipo nafasi ya pili kutoka chini kwenye msimamo ikiwa na pointi 23 hivyo kama watapoteza mchezo huo watakuwa kwenye hali mbaya zaidi.

Mchezo huo utakuwa ni wa 27 hivyo itasalia na mechi tatu ambazo zitaamua kama wanashuka daraja au wanabaki.

Msemaji wa klabu hiyo, Idrissa Bandari amesema wanaiheshimu Simba kutokana na ubora iliyonayo kwa sasa lakini watapambana kuhakikisha wanapata pointi tatu ili kujikwamua.

"Tunahitaji sana kupata pointi tatu, hatupo kwenye hali nzuri, wachezaji wanalijua hilo lakini tunajua Simba ni timu bora ila tutaingia uwanjani kutafuta pointi tatu," alisema Bandari.

Simba inahitaji pointi tatu ili kujihakikishia kuchukua ubingwa msimu huu kitu ambacho kinaufanya mchezo huo utakaofanyika uwanja wa Taifa saa 10 jioni kuwa na ushindani mkubwa.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top