Timu ya Taifa ya Wanawake wa Tanzania 'Twiga Stars' imetolewa kwenye michuano ya kufuzu fainali za Afrika baada ya kulazimishwa sare ya bao moja timu ya Zambia 'Shepolopolo'.
Katika mchezo wa kwanza uliofanyika hapa jijini Dar es Salaam wiki iliyopita Twiga ililazimiahwa sare ya mabao 3-3 na Shepolopolo.
Hii ina maana timu hizo zimetoka sare ya mabao 4-4 lakini Twiga imeondosha baada ya kuruhusu magoli mengi nyumbani.
Timu za Tanzania zimekuwa zikishindwa kutumia vizuri uwanja wa nyumbani na kijitutumua ugenini hali inayosababisha kutupwa nje ya michuano mbalimbali.
Bao pekee la Twiga lilifungwa na Donisia Daniel.
TWIGA STARS YATOLEWA SHEPOLOPOLO AFRIKA
Title: TWIGA STARS YATOLEWA SHEPOLOPOLO AFRIKA
Author: SDF SPORTS
Rating 5 of 5 Des:
Author: SDF SPORTS
Rating 5 of 5 Des:
Timu ya Taifa ya Wanawake wa Tanzania 'Twiga Stars' imetolewa kwenye michuano ya kufuzu fainali za Afrika baada ya kulazimishwa sa...
Post a Comment