SDF SPORTS SDF SPORTS Author
Title: AZAM YASHINDWA KUISHUSHA YANGA YAKOMALIWA SOKOINE
Author: SDF SPORTS
Rating 5 of 5 Des:
Azam FC imeshindwa kukwea hadi nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi baada ya kulazimishwa sare ya bila kufungana na Mbeya City kwenye u...
Azam FC imeshindwa kukwea hadi nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi baada ya kulazimishwa sare ya bila kufungana na Mbeya City kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.

Azam yenye pointi 45 ingeshinda ingefikisha alama 48 na kuishusha Yanga ambapo ingeizidi alama mbili na kudiwa moja na vinara Simba.

Azam wameingia kwenye mchezo huo wakiwa na kumbukumbu ya kutolewa kwenye michuano ya FA na Mtibwa Sugar mwisho wa mwezi uliopita.

Katika mchezo wa leo Azam ilitengeneza nafasi kadhaa huku mshambuliji Shaban Idd akipoteza ya wazi kipindi cha kwanza.

Wenyeji City walitengeneza mashambulizi kupitia upande wa kushoto lakini hawakufanikiwa kupata bao.

City imeendelea kubaki nafasi ya nane kwenye msimamo ikiwa na pointi zake 26.

Matokeo ya mechi nyingine za VPL zilizochezwa leo

Stand United 3-1 Njombe Mji
Ruvu Shooting 0-0 Tanzania Prisons
Ndanda FC 1-1 Kagera Sugar

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top