SDF SPORTS SDF SPORTS Author
Title: MATOLA: MBAO WANA HALI NGUMU LAKINI LEO WATATUSAMEHE
Author: SDF SPORTS
Rating 5 of 5 Des:
Kocha msaidizi wa timu ya Lipuli FC, Suleiman Matola amesema wana tegemea kupata upinzani mkubwa kutoka kwa wenyeji wa Mbao FC katika mc...

Kocha msaidizi wa timu ya Lipuli FC, Suleiman Matola amesema wana tegemea kupata upinzani mkubwa kutoka kwa wenyeji wa Mbao FC katika mchezo wa ligi kuu hii leo lakini wao ndio wataibuka na ushindi.

Nahodha huyo wa zamani wa timu ya Simba amesema Mbao wapo kwenye nafasi mbaya kwenye msimamo wa ligi na wanafahamu watapambana kufa na kupona kupata alama tatu lakini leo itakuwa ngumu kwao.

Mchezo huo utafanyika saa 10 jioni katika uwanja wa CCM Kirumba ambao unatarajiwa kuwa wavute nikuvute kwa timu zote.

Mbao wamekuwa wakicheza vizuri sana wanapokuwa katika uwanja huo na kuwapa shida wapinzani wao kitu ambacho Lipuli wanatarajia kitatokea.

"Mbao wapo nafasi ya pili kutoka chini, tunafahamu watataka kupata ushindi wa nyumbani ili kujinasua ingawa leo tutawafunga," alisema Matola kwa kujiamini.

Lipuli ipo nafasi ya saba kwenye msimamo ikiwa na pointi 27 wakati Mbao ikiwa nafasi ya 14 na alama zake 19.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top