Azam FC imesema
itaingia katika mchezo wa kombe la FA dhidi ya timu ya Manispaa ya Kinondoni
(KMC) utakaofanyika leo jioni ikiwa na lengo moja la kushinda ili kufuzu
hatua ya robo fainali.
Mchezo huo utaanza saa
1 jioni katika kwenye uwanja wa Azam Complex huku KMC ikiwa mwenyeji wa Wana lamba lamba hao
Msemaji wa klabu hiyo,
Jaffer Idd amesema wanafahamu kuwa mchezo huo utakuwa mgumu na wanawaheshimu
wapinzani wao lakini kesho wajiandae kutolewa kwenye michuano hiyo.
Jaffer amesema
wachezaji wote wapo kwenye hali nzuri isipokuwa wataendelea kukosa huduma ya
nahodha wao Himid Mao ambaye amerejea kutoka Afrika Kusini kupata matibabu ya
goti.
"Michuano ya FA
siku zote haina sare wala marudiano lazima mmoja afungwe nasi tunalijua ndio
maana tumejipanga kuhakikisha tunashinda na wachezaji wametuahidi hilo.
"Maandalizi
yalianza toka Jumatatu kwahiyo benchi la ufundi chini ya Aristica Cioba
linasema kila kitu kimeenda sawa na wachezaji wapo tayari kwa mchezo,"
alisema Jaffer.
Post a Comment