SDF SPORTS SDF SPORTS Author
Title: AZAM YAHOFIA KUNG'ANG'ANIWA NA RUVU SHOOTING, JUMAMOSI
Author: SDF SPORTS
Rating 5 of 5 Des:
Pamoja na Maafande wa Ruvu Shooting kuwa mkiani katika msimamo wa ligi kuu timu ya Azam FC itaingia kwa tahadhari kubwa katika mchezo dhi...
Pamoja na Maafande wa Ruvu Shooting kuwa mkiani katika msimamo wa ligi kuu timu ya Azam FC itaingia kwa tahadhari kubwa katika mchezo dhidi yao utakaofanyika siku ya Jumamosi.

Timu hizo zitakutana katika uwanja wa Azam Complex katika mchezo ambao Ruvu wataingia kwa nguvu kusaka alama tatu ili kujinasua mkiani.

Ofisa habari wa Azam FC, Jaffer Idd amesema kucheza na timu inayohitaji pointi kujinasua mkiani ni ngumu kwa sababu wanatumia nguvu kubwa ingawa wao wamejipanga kukabiliana nao kwa kila hali.

"Tunawaheshim Ruvu, wapo mkiani lakini hilo halitupi kujiamini kuwa tutawafunga, tumejiandaa vizuri kuhakikisha tunatoka na pointi zote kwenye uwanja wetu wa nyumbani ligi ni ngumu sana msimu huu," alisema Jaffer.

Jaffer amesema pia walikuwa na mchezo wa kirafiki jana usiku dhidi ya Ashanti United ili kukiweka sawa kikosi chao kabla ya kuwakabili Ruvu mwishoni mwa juma.

"Tulicheza na Ashanti jana tukawafunga mabao 4-0. Mabao yalifungwa Idd Kipagwile, Enock Atta Agyei, Waziri Junior na David Mwantika," alimalizia Jaffer.

Azam ipo nafasi ya nne ikiwa na pointi 16 wakati Ruvu ina alama zake tano mkiani.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top