SDF SPORTS SDF SPORTS Author
Title: MANARA: SIMBA TUNAHUJUMIWA
Author: SDF SPORTS
Rating 5 of 5 Des:
Mkuu wa kitengo cha habari na mawasiliano wa klabu ya Simba, Hajji Manara amelalamika kuwa waamuzi wamekuwa wakiwahujumu katika mchezo ya...
Mkuu wa kitengo cha habari na mawasiliano wa klabu ya Simba, Hajji Manara amelalamika kuwa waamuzi wamekuwa wakiwahujumu katika mchezo yao ya ligi.

Manara amesema kuwa wameandika barua kwa bodi ya ligi (TPLB) kuhusu malalamiko yao ambapo katika michezo dhidi ya Mbao walinyimwa penati mbili, Stand United ilipewa penati isiyo halali na katika mechi ya Yanga pia walinyimwa penati mbili.

Manara amewaonyesha picha za video Waandishi wa habari kuhusu matukio mbalimbali yaliyojitokeza katika michezo yao mitatu iliyopita na kuwataka waamuzi kuchezesha kwa kufuatia sheria 17 za soka.

"Tumeandika barua kwa bodi ya ligi kutoa malalamiko yetu kuhusu hujuma dhidi yetu, waamuzi wamekuwa wakitunyima penati tunataka mpira uchezeshwe kwa haki," alisema Manara.

Msemaji huyo alisema anajua kauli hiyo inaweza kumuweka matatani na pia kumfanya kufungiwa lakini hilo halimtishi na anatetea kibarua chake.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top