SDF SPORTS SDF SPORTS Author
Title: KAGER SUGAR KUIBUKIA KWA AZAM LEO..? RATIBA YOTE VPL IKO HAPA
Author: SDF SPORTS
Rating 5 of 5 Des:
Mzunguko wa Tatu wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), inatarajiwa kuendelea leo na wikiendi yote Azam FC itaialika Kagera Sugar sa...
Mzunguko wa Tatu wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), inatarajiwa kuendelea leo na wikiendi yote
Azam FC itaialika Kagera Sugar saa 1.00 usiku (19h00) katika Uwanja wa Azam ulioko Chamazi jijini Dar es salaam.
Kesho Jumamosi Mabingwa watetezi  Young Africans mgeni wa Majimaji FC ya Songea saa 10.00 jioni (16h00) katika Uwanja wa Majimaji mkoani Ruvuma.
Mbao itasafiri hadi Manungu mkoani Morogoro kucheza na Mtibwa Sugar katika mchezo ambao pia utapigwa Jumamosi saa 16h00 wakati Tanzania Prisons ya Mbeya itakuwa mwenyeji wa Ndanda FC saa 16h00 kwenye Uwanja wa Sokoine.
Lipuli Fc itakuwa mwenyeji wa Ruvu Shooting saa 16h00 katika Uwanja wa Samora, Iringa wakati Stand United itacheza na Singida United saa 16h00 kwenye Uwanja wa Kambarage, Shinyanga.
Siku ya Jumapili Septemba 17, 2017 Mbeya City itaikaribisha Njombe Mji saa 16h00 kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya huku Simba SC ikiwa mwenyeji wa Mwadui FC saa 16h00 jioni katika Uwanja wa Uhuru, Dar es salaam.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top