Mhe. Mwakyembe amewaasa vijana wa Serengeti kuliwakilisha
vyema Taifa kwenye michuano ya AFCON wanayotarajia kwenda kushiriki hivi
karibuni.
Mhe. Mwakyembe akiongozana na Rais wa Shirikisho la Mpira
wa Miguu Tanzania (TFF), Bw. Jamal Malinzi aliwahakikishia vijana wa
Serengeti utayari wa Serikali katika kuendeleza mpira wa miguu nchini.
Vilevile, Mhe. Mwakyembe ametoa rai kwa Watanzania
kuendelea kuwachangia Serengeti Boys ili waweze kuwa na ushiriki bora
katika michezo ya maandalizi nchini Morroco na Cameroun na baadaye
katika michuano ya AFCON, nchini Gabon.
Sambamba na hilo Mhe. Mwakyembe aliwaongoza wananchi
waliofika uwanja wa Taifa kuishangilia Serengeti boys iliyokuwa ikicheza
mechi ya kirafiki na timu ya Taifa ya vijana kutoka Ghana, ambapo
Serengeti boys wameweza kurudisha magoli mawili na matokeo hadi mwisho
yakawa sare ya 2-2.
Post a Comment