Wekundu wa Msimbazi Simba Sports Club
wameiomba Serikali kuingili swala Kagera Sugar kupokwa pointi tatu kwa
kumchezesha beki Mohammed Fakhi ambaye alikuwa na kadi tatu za njano.
Msemaji
wa klabu hiyo Haji Manara amesema Kamati ya masaa 72 chini ya
Mwenyekiti wake Hamad Yahaya iliipa Simba pointi tatu kufuatia baada ya
kujiridhisha kuwa mchezaji Fakhi alikuwa na kadi tatu za njano.
Kamati
ya katiba sheria na hadhi haina mamlaka ya kupitia shauli hili kwa kuwa
maamuzi yanatolewa na bodi yenyewe ya ligi na wala sio kamati hiyo
wamesema Manara
Kamati ya
Bodi ya Ligi chini ya Mwenyekiti wake Hamad Yahaya ilishatoa maamuzi na
ilijiridhisha kuwa mchezaji Fakhi ana kadi Tatu za njano
Haijawahi kutokea mchezaji aliyepewa kadi anaitwa kuitwa kuhojiwa amesema Manara
Manara
amesema wanawapa TFF mpaka jumatatu wawe wametoa maamuzi yote ya kesi
mbalimbali wamechoka kuonewa sasa. na yupo tayari kufungiwa baada ya
press yake ya leo.


Post a Comment