SDF SPORTS SDF SPORTS Author
Title: DROO YA KOMBE LA SHIRIKISHO KUPANGWA KESHO
Author: SDF SPORTS
Rating 5 of 5 Des:
Mabingwa watetezi wa kombe la ligi kuu ya soka Tanzania Bara, Yanga, kesho wanatarajia kufahamu ni timu gani itakayopambana nayo katika...
Mabingwa watetezi wa kombe la ligi kuu ya soka Tanzania Bara, Yanga,
kesho wanatarajia kufahamu ni timu gani itakayopambana nayo katika mechi mbili za mtoano ili kupata nafasi ya kuingia katika hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Barani Africa, wakati ratiba ya mechi hizo itakapopangwa hapo kesho katika Makao Makuu ya CAF yaliyoko Cairo nchini Misri.

Mzunguko huo wa timu 16 itakutanisha timu zilizoondolewa kwenye hatua ya pili ya Ligi ya Mabingwa Barani Africa na timu zilizofuzu katika hatua hiyo ya kwanza kwa mwaka 2017 kutoka kombe la shirikisho.
Yanga inaenda kwenye Kombe la Shirikisho baada ya kutolewa kwa sheria ya goli la ugenini na Zanaco ya Zambia, baada ya suluhu ya bila kufungana katika mechi iliyofanyika juzi nchini Zambia. 

Timu zingine zilizoangukia kwenye Kombe la Shirikisho ni RC Kadiogo (Burkina Faso), AC Leopards (Congo), AS Tanda (Cote d’Ivoire), TP Mazembe (DR Congo), Mounana (Gabon), Gambia Ports Authority (Gambia), Horoya (Guinea), CNaPS (Madagascar), AS Port Louis (Mauritius), FUS Rabat (Morocco), Barrack Young Controllers (Liberia), Rivers United, Rangers (Nigeria), Bidvest (South Africa),

Wakati timu zilizofuzu kutoka katika hatua ya kwanza ya kombe la shirikisho ni MC Alger, JS Kabylie (Algeria), Recreativo do Libolo (Angola), ASEC Mimosas (Cote d’Ivoire), El Masry, Smouha (Egypt), MAS Fes, Ittihad Tangier (Morocco), Rayon Sports (Rwanda), Hilal El Obeid (Sudan), Mbabane Swallows (Swaziland), Platinum Stars, Supersport (South Africa), Club Africain, CS Sfaxien (Tunisia), Zesco United (Zambia). 

Mechi za kwanza zitapigwa kati ya tarehe 7-9 April na mechi za marudiano zitakuwa kati ya tarehe 14-16 April.


Kila la kheri wawakilishi pekee wa Tanzania katika michezo ya vilabu barani Africa

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top