SDF SPORTS SDF SPORTS Author
Title: SERENGETI BOYS YABAKIZA MGUU MMOJA KUINGIA KOMBE LA DUNIA
Author: SDF SPORTS
Rating 5 of 5 Des:
Timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys jana imeibuka na ushindi wa kwanza katika Fainali za Vijana Afrika ...


Timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys jana imeibuka na ushindi wa kwanza katika Fainali za Vijana Afrika chini ya umri wa miaka 17 dhidi ya Angola kwa bao 2-1

Ikicheza kwenye uwanja wa L'Amitie mjini Libreville Serengeti boys walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia Kevin Naftal katika dakika ya 4 kabla ya Chilumbo kusawazisha, mpaka mapumziko Tanzania 1-1 Angola 

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku timu zote zikishambuliana Serengeti boys walikosa umakini katika kumalizia mashambulizi, dakikia ya 69 Abdul Suleiman aliwainua ma elfu ya mashabiki wa Tanzania kwa kupiga bao safi kabisa baada ya kupokea pasi ya Mkomola

Tanzania anaongoza kundi B pointi 4 akifuatiwa na mali mwenye point 4 pia

Karata ya mwisho kwa Tanzania itakuwa dhidi ya Niger ili kujihakikishia nafasi katika nusu fainali na baadae Kombe la Dunia

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top