Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) inatarajiwa kuendelea kesho Jumamosi Oktoba 15, 2016 kwa michezo mitatu ambako Simba inayoongoza katika msimamo wa kuwania taji hilo katika timu 16 itaikaribisha Kagera Sugar ya Kagera kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Katika mchezo huo Na.73, mwamuzi atakuwa Hussein Athuman kutoka mkoani Katavi ambako pembeni atasaidiwa na Joseph Bulali wa Tanga na Silvester Mwanga wa mkoani Kilimanjaro wakati Soud Lila wa Dar es Salaam atakuwa mwamuzi wa akiba huku Kamishna wa mchezo akiwa Pius Mashera wa Dodoma.
Mchezo mwingine utakuwa ni kati ya JKT Ruvu na Mwadui ya Shinyanga. Ni mchezo Na. 74 utakaofayika Uwanja wa Mabatini ulioko Mlandizi mkoani Pwani ambako utachezeshwa na Mwanamama mwamzi mwenye beji la FIFA, Mwanahamisi Matiku wa Dar es Salaam, akisaidiwa na Shafii Mohamed pia wa Dar es Salaam na Gesper Ketto wa Arusha.
Mwamuzi wa akiba atakuwa Abdallah Rashid wa Pwani wakati Kamishna wa mchezo huo atakuwa Charles Mchau wa Kilimanjaro.
Pia Stand United ya Shinyanya itaikaribisha African Lyon kwenye Uwanja wa CCM Kambarage katika mchezo Na. 75 ambao utachezeshwa na Eric Onoka wa Arusha akisaidiwa na Agnes Pantaleo pia wa Arusha na Omary Juma wa Dodoma wakati mwamuzi wa akiba atakuwa Joseph Pombe wa Shinyanga. Kamishna wa mchezo atakuwa Hamisi Kitila wa Singida.
Mola jaalia Simba sc tuondoke na ushindi mnono hapo kesho.Amiin.
ReplyDelete