Singida United imeiweka Njombe Mji mguu sawa kuelekea kushuka daraja msimu huu baada ya kukubali kipigo cha mabao 4-0 mtanange uliofanyika uwanja wa Namfua.
Njombe ipo mkiani mwa msimamo wa ligi ikiwa na pointi 22 na imeshuka dimbani mara 27 ikisalia na mechi tatu pekee.
Mshambuliaji Salita Kambale aliifungia Singida bao la kwanza dakika ya 43 baada ya kazi nzuri ya Lubinda Mundia.
Mlinzi Miraji Adam aliifungia Singida bao la pili kwa mkwaju penati ya 59 kabla ya Mundia kuongeza la tatu dakika mbili baadae.
Nahodha Nizar Khalifan aliwapatia wenyeji bao la nne dakika za lala salama baada ya kutoka benchi kuchukua nafasi ya Mudathir Yahya.
Singida imefikisha pointi 41 na kuendelea kubaki nafasi ya tano baada ya Tanzania Prisons kupata ushindi wa bao moja dhidi ya Lipuli FC.
SINGIDA YAZIDI KULIZAMISHA JAHAZI LA NJOMBE MJI
Title: SINGIDA YAZIDI KULIZAMISHA JAHAZI LA NJOMBE MJI
Author: SDF SPORTS
Rating 5 of 5 Des:
Author: SDF SPORTS
Rating 5 of 5 Des:
Singida United imeiweka Njombe Mji mguu sawa kuelekea kushuka daraja msimu huu baada ya kukubali kipigo cha mabao 4-0 mtanange uliofanyika...


Post a Comment