SDF SPORTS SDF SPORTS Author
Title: MATUKIO KWA PICHA SIMBA WALIPOMTANGAZA MSHINDI WA ZABUNI
Author: SDF SPORTS
Rating 5 of 5 Des:
Msajili wa vyama vya michezo na vilabu (kushoto) akimwakilisha waziri wa habari, sanaa, utamaduni na michezo. Kulia ni kaimu rais wa kla...
Msajili wa vyama vya michezo na vilabu (kushoto)
akimwakilisha waziri wa habari, sanaa, utamaduni na michezo.
Kulia ni kaimu rais wa klabu ya Simba


Mwenyekiti wa kamati ya Zabuni Jaji mtaafu Thomas Mihayo
akiwasalimu wanachama wa Simba kabla ya kumtangaza
mshindi wa zabuni ya uwekezaji ndani ya klabu ya Simba

Makamu wa rais wa Shirikisho la mpira Tanzania
Michael Richard Wambura akiliwakilisha shirikisho hilo
katika mkutano wa Simba

Kulia ni mwanachama wa Simba, Bi. Hindu aliyekuwa
akipinga kwa nguvu zote mabadiliko katika klabu hiyo akifuatilia
kwa makini mkutano wa kumtangaza mshindi wa zabuni

Wanachama wa Simba walilipuka kwa shangwe mara
baada ya kutangaziwa jina la mshindi wa zabuni ya
uwekezaji ndani ya klabu yao.

Msemaji wa Simba Haji Manara (mwenye suti kushoto)
akimkaribisha ukumbini mfanyabiashara Mohammed Dewji
(aliyepunga mikono miwili) mara baada ya jina lake kutangazwa mshindi wa zabuni

Mohammed Dewji 'MO' akiwasalimu wanachama wa Simba
mara tu alipotangazwa mshindi wa zabuni na kuingia ukumbini

MO akisalimiana na kaimu rais wa Simba Salim Abdallah 'TRY AGAIN'

MO akisalimiana na katibu wa kamati ya
zabuni Bi. Brenda Mrema

Mohammed Dewji akiwashukuru wanachama kabla ya
kukaa mara baada ya kuingia ukumbini


MO akiwa amekaa katikati ya mgeni rasmi kulia na
kushoto ni mwenyekiti wa kamati ya zabuni

MO Dewji alipokuwa akiwaeleza wanachama mipango
ya muda mrefu na mfupi ndani ya klabu ya Simba mara
baada ya kushinda zabuni

MO akipeleka ujumbe kwa wachezaji watakaoichezea klabu
ya Simba kutambua thamani kubwa ya kuvaa jezi ya timu hiyo uwanjani


Mo akipeana mikono na mgeni rasmi baada ya kuelezea
mipango yake ndani ya Simba

Mwanachama wa Simba akiserebuka baada ya kusikia
mipango ya muda mrefu na mfupi kutoka kwa mwekezaji MO

Ilikuwa ni shangwe tupu ndani ya ukumbi wa Mwl Nyerere,
wanasimba wakifurahia mipango ya mwekezaji katika timu yao


Salim Abdallah "Try Again" kaimu rais wa Simba aliyeongoza
kwa uweledi wa hali juu mchakato wa mabadiliko katika klabu ya Simba

MO akionekana mwenye furaha kubwa mara baada ya mchakato
wa uwekezaji kukamilika kwa zaidi ya asilimia 99.99

Makamu wa rais wa TFF, Mwenyekiti wa
kamati ya zabuni na mshindi wa zabuni

Makamu wa rais wa TFF akiteta jambo na Mo wakati
mkutano ukielekea kuisha


Jaji Mtaafu Thomas Mihayo akifurahia jambo na Mohammed Dewji

Mwanasheria Msomi na aliyewahi kuwa katibu mkuu wa
Simba Evodius Mtawala akifafanua hatua zinazofuata baada ya
kutangazwa mshindi wa zabuni ya uwekezaji katika klabu ya Simba

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top