SDF SPORTS SDF SPORTS Author
Title: CHEKI SAMATA ANAVYOITANGAZA TANZANIA NCHINI UBELGIJI
Author: SDF SPORTS
Rating 5 of 5 Des:
Nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania, Mbwana Samata ameendelea kupeperusha vema bendera ya nchi baada ya mashabiki wa timu yake ya KRC G...
Nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania, Mbwana Samata ameendelea kupeperusha vema bendera ya nchi baada ya mashabiki wa timu yake ya KRC Genk kubeba mabango yenye picha yake akiwa na jezi ya Stars kutokana na uwezo anao uonyesha kwa sasa.

Samata amekuwa akiisaidia Genk kufanya vizuri hata asipofanikiwa kufunga bao anaonyesha uwezo na kusaidia wenzie kufunga.

Katika mchezo wa juzi Jumatano walioibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Club Brugge, Samata alifunga bao la pili dakika ya 90 kwa shuti kali hali iliyoamsha shangwe uwanja mzima.

Mashabiki wa Genk walionyesha bango la nahodha huyo akiwa na jezi ya Stars ikiwa ndani ya bendera ya Tanzania na kuitangaza nchini huko Ubelgiji.

Genk iko nafasi ya saba kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi 17 alama 13 nyuma ya vinara Brugge.

About Author

Advertisement

Post a Comment

  1. UKIWA UWANJANI MTU HUWA NA FARAJA SANA ASA PALE UNAPOONA TANZANIA INAPOTANGAZWA NA KUJULIKANA.

    ReplyDelete

 
Top