SDF SPORTS SDF SPORTS Author
Title: SIMBA: OMOG NI WA HAPA HAPA HAONDOKI NG'O
Author: SDF SPORTS
Rating 5 of 5 Des:
Uongozi wa klabu ya Simba bado una imani na kocha Joseph Omog na hawajampa mechi yoyote ili wamtimue. Kaimu Rais wa klabu hiyo Salim Abd...
Uongozi wa klabu ya Simba bado una imani na kocha Joseph Omog na hawajampa mechi yoyote ili wamtimue.

Kaimu Rais wa klabu hiyo Salim Abdallah 'Try Again' alikutana na kocha  huyo  raia wa Cameroon jana  baada ya kumalizika kwa mchezo dhidi ya Mwadui FC  na kumuhakikishia nafasi bado ipo  ndani ya Wekundu hao.

Msemaji wa timu hiyo Hajji Manara amewaambia Waandishi kuwa Mashabiki wanamekuwa wakimpigia kelele kocha huyo ila Uongozi hauko tayari kumuacha kocha huyo.

"Mashabiki wa Simba sijui wanataka  nini timu inafanya  vizuri lakini hawamtaki kocha.

"Simba imecheza mechi tisa bila kufungwa hata bao  moja  lakini kwa sasa kila mtu  anajifanya  kocha ila  Omog haondoki," alisema Manara.

Manara alisema kikosi kamili cha Simba kitaondoka Kesho kuelekea jijini Mwanza  kwa ajili ya mchezo dhidi ya Mbao siku ya Alhamisi.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top