SDF SPORTS SDF SPORTS Author
Title: MBAO YAIPUNGUZA KASI SIMBA YAILAZMISHA SARE KIRUMBA
Author: SDF SPORTS
Rating 5 of 5 Des:
Timu ya soka ya Simba imeshindwa kuendelea wimbi la ushindi baada ya kulazimishwa sare timu ya Mbao fc ya bao 2-2 katika uwanja wa Ccm Ki...
Timu ya soka ya Simba imeshindwa kuendelea wimbi la ushindi baada ya kulazimishwa sare timu ya Mbao fc ya bao 2-2 katika uwanja wa Ccm Kirumba Jijini Mwanza

Simba walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa winga wake Shiza Kichuya mapema katika dakika ya 16 baada ya kuunganisha vyema krosi ya Erasto Nyoni, mpaka mapumziko Simba walikuwa mbele kwa bao 1-0

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na Mbao kusawazisha kupitia kwa Habibi kiyombo katika dakika ya 46, Simba walicharuka iliwachukua dakika mbili James Kotei akaipatia Simba goli la pili.
Zikiwa zimesalia dakika 10 beki Boniface Maganga alisawazishia Mbao kwa goli zuri kabisa katika dakika ya 81 kwa kuupiga mpira uliomshinda Kipa Manua mpaka dakika 90 Mbao 2-2 Simba

Simba walifanya mabadiliko kwa kuwatoa Shiza Kichuya na Asamoah Gyan nafasi zao zikachukuliwa na Haruna Niyonzima na Juma Luizio


Simba wamefikisha Pointi 8 baada ya kushinda 2 na kusuluhu 2, Mechi ijayo Simba atakuwa Shinyanga dhidi ya Stand United siku ya tarehe 1 oktoba

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top