SDF SPORTS SDF SPORTS Author
Title: KICHUYA FITI KUIVAA STAND UNITED
Author: SDF SPORTS
Rating 5 of 5 Des:
Uongozi wa timu ya soka ya Simba SC umesema mchezaji wao Shizya Kichuya yuko tayari kwajili ya mchezo wao wa Jumapili ambapo timu hiyo it...
Uongozi wa timu ya soka ya Simba SC umesema mchezaji wao Shizya Kichuya yuko tayari kwajili ya mchezo wao wa Jumapili ambapo timu hiyo itavaana na Stand united mkoani Shinyanga katika uwanja wa CCM Kambarage.

Akizungumza katika mahojiano maalumu Mratibu wa klabu ya Simba SC Abass Suleiman alisema mchezaji wao Shiza Kichuya yuko njema na anatarajia kucheza dhidi ya Stand united.

Abass alisema Kichuya alianza mazoezi tokea siku ya Jumatatu na siku za Jumanne na Jana,Kichuya amekuwa akifanya mazoezi na wenzake.
Mratibu huyo alisema timu yao ilicheza mchezo wa kirafiki mkoani Tabora ambapo timu hiyo ilipata sare ya bila kufungana dhidi ya Mirambo.

Akielezea mchezo huo,Abass alisema timu yao ilitumia mchezo huo kama sehemu ya kurekebisha makosa yao yaliojitokeza dhidi ya mchezo wao na Mbao FC.

Akielezea kuhusu hali za wachezaji Said Mohamed’Nduda’ na Shomari Kapombe,Abass alisema Ndunda ataondoka nchini Jumapili kwenda India kwajili ya matibabu.

Abass alisema Nduda atakuwa India siku 4 za matibabu kisha atarejea nchini na baada ya wiki 4,kipa huyo atanza mazoezi.

Kwa upande wa hali ya mchezaji Kapombe,Abass alisema Kapombe ameanza mazoezi mepesi na anatarajia kujiunga na timu yao itakaporejea Dar-es-salaam

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top