SDF SPORTS SDF SPORTS Author
Title: IRINGA ACADEMY YAANZA KUTOA MATUNDA
Author: SDF SPORTS
Rating 5 of 5 Des:
Uongozi wa Iringa football academy unapenda kutoa taarifa juu ya vijana wao wanne kuitwa katika majaribio katika timu ya taifa ya vijana ...
Uongozi wa Iringa football academy unapenda kutoa taarifa juu ya vijana wao wanne kuitwa katika majaribio katika timu ya taifa ya vijana (u17) vijana wawili walichujwa na wawili waliweza kuendelea na mazoezi pale uwanja wa karume chini ya kocha mkuu wa vijana Kim Poulsen

Iringa football academy inatoa shukrani za dhati kwa uongozi wa TFF pamoja na benchi zima la ufundi kwa kutoa nafasi ya kupeleka vijana wao, pia inatoa shukrani za dhati kwa wazazi na walezi kwa kutoa ruhusa kwa vijana wao kwenda kuonesha vipaji vyao ili kulipigania taifa leo.
Kambi ya viajana hao ilikuwa ya mwezi mmoja na imevunjwa rasmi juzi


Kikosi hiko cha vijana kinaandaliwa kwa ajili ya mashindano ya u17 yatakayofanyika mwaka 2019 Tanzania ndio mwenyeji wa mashindano hayo

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top