SDF SPORTS SDF SPORTS Author
Title: FAINALI KOMBE LA FA NGOMA KUPIGWA DODOMA
Author: SDF SPORTS
Rating 5 of 5 Des:
Baada ya Jana kuenea kwa taarifa iliyoripotiwa kuwekwa na Rais wa TFF Jamal malinzi juu ya kufanya droo ya kujua uwanja gani utatumik...


Baada ya Jana kuenea kwa taarifa iliyoripotiwa kuwekwa na Rais wa TFF Jamal malinzi juu ya kufanya droo ya kujua uwanja gani utatumika kwa fainali ya kombe hilo baina ya Simba na Mbao,hatimaye Leo TFF imekata mzizi wa fitna baada ya kutangaza kwamba mechi hiyo itapigwa dodoma tarehe 28/05/2017.

Mashabiki wengi wa soka nchini walionekana kushtushwa na taarifa aliyotoa malinzi kupitia mtandao wake wa Twitter juu ya kufanyika kwa droo hiyo ambapo walisema hakuna utaratibu kama huo duniani,lakini wakati mashabiki wa soka wakisubiri kuona kufanyika kwa droo hiyo ghafla taarifa ikatolewa na TFF Leo hii kwamba mechi hiyo itafanyika Mjini Dodoma.

Simba na mbao zilingia fainali baada ya kuzifunga azam na yanga kwa goli 1-0,hivyo kuzifanya timu hizo kukutana kuamua nani atawakilisha nchi kwenye kombe la shirikisho barani Africa mwakani.

Mbao imeweka historia kuwa timu iliyopanda daraja na kuja kufanya makubwa katika soka.la Tanzania kwa kuweza kuvitingisha vigogo kama.simba,yanga,azam,mtibwa sugar nk

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top