SDF SPORTS SDF SPORTS Author
Title: WEEKEND YA KIBABE BONGO HADI ULAYA
Author: SDF SPORTS
Rating 5 of 5 Des:
Bongo kuna nyimbo ya mkongwe wa bongo flavor anaefahamika kama professor Jay au Joseph Haule inaitwa Show ya Kibabe,nadhani ni jina sahih...

Bongo kuna nyimbo ya mkongwe wa bongo flavor anaefahamika kama professor Jay au Joseph Haule inaitwa Show ya Kibabe,nadhani ni jina sahihi linaloweza kuielezea wiki hii ilomalizika maana kulifanyika mambo ya kibabe ndani na nje ya viwanja vya michezo.

Tiririka chini hapa uone ubabe wenyewe.

Tanzania
Inawezekana ikawa kuna mengi yametokea lakini kubwa zaidi ilikuwa ni sakata la rufaa ya klabu ya Simba iliyokubaliwa na kamati inayosimamia ligi kuu Tanzania almaarufu kama kamati ya masaa 72,lakini kamati ya katiba sheria na hadhi za wachezaji ikaingilia kati na kuitisha kikao cha kupitia maamuzi hayo,sakata likachukua sura mpya,kila neno likasemwa hadi kufikia msemaji wa Simba Haji Manara kuitisha mkutano na wanahabari ili kuonesha masikitiko ya klabu juu ya muenendeo wa TFF na mambo mbalimbali yaliyoihusu au yanayoihusu Simba,ebana eeh manara akaongea kibabe,TFF wakamsikia,wakamtia hatiani na kumpeleka kwenye kamati ya maadili,manara akajibu kibabe ntaenda kubutua,wakakubaliana jumanne kwa maana kesho aitwe kuhojiwa,unajua kilichotokea,kamati ikabutua kibabe na kumbutua manara bila kumsikiliza na kumpiga mvua moja na kubwa kuliko wakampiga na faini la kibabe la mil 9,tunasubiria jibu la kibabe kutoka kwa manara.

Wakati manara anapigwa ban mapema mashabiki wa mpira kabla hawajakaa sawa wakapokea taarifa nyingine ya kibabe,eeh Simba imepokonywa point walizopewa na kamati ya masaa 72,wanamsimbazi wakapagawa lakini unajua kilichowapagawishEti maamuzi ya kamati ya saa 72 hayakuwa sahihi kwa sababu zifutazo.
1. Simba iliwakilisha rufaa hiyo nje ya muda.
2. Simba haikulipia ada ya kukatia rufaa ambayo ni pesa madafu kama laki 3.
3. Kali nyingine eti kamati ya saa 72 haikuwa halali kutoa maamuzi hayo sababu kuna wajumbe walishiriki ambao hawakuwa na haki ya kushiriki hivyo maamuzi yao yalikuwa batili.
Hahaa yote kwa yote maamuzi haya nayo yalikuwa yakibabe tu.

Yanga nayo ilitolewa kwenye michezo ya kimataifa ikaipiga kibabe prison kwenye robo fainali ya kombe la FA maarufu kama.Azam.confederation cup, kisago cha kibabe cha bao 3-0 kikawatoa prison na kuipeleka yanga Mwanza kukumbana na Wazee wa mbao,huku game la kibabe la nusu fainali likipigwa Dsm.kati ya mjeruhiwa wa point Simba dhidi ya waoka mikate wa azam.
Weekend ya kibabe kwa bongo iliishia kwa mwanariadha simbu kushika nafasi ya 5 huko kwenye mashindano ya London Marathon,si haba simbu.

Ah nilitaka kusahau,Serengeti boys ikawabutua kibabe Gabon ambao ndio wenyeji wa kombe la mataifa ya Africa kwa vijana baadae mwezi mei kwa bao 2-1 katika mechi ya kirafiki.

Ulaya

Ubabe haukuishia bongo tu,ulaya pia kulikuwa na show za kibabe,uingereza Chelsea ikaipiga spurs goli 4-2 katika nusu fainali ya Fa,baada ya hapo arsenal nao wakaibutua man city katika nusu fainali nyingine ya fa kwa goli za kibabe 2-1,kwahyo fainali itakuwa kati ya wababe wa London, Chelsea vs Arsenal
Man united ikiwa na kumbukumbu ya kutopata goli katika uwanja wa turf mor unaomilikiwa na Burnley kwa muda wa miaka 41,iliingia kibabe na kuifumua Burnley kwa goli 2 -0,
Hatujakaa sawa Huko anfield, wageni crystal palace waliingia kibabe na kuibutua Liverpool kwa magoli mawili yakikatili yalotiwa kambani na mshambuliaji wa zamani wa Liverpool Christian benteke,lakini kwa heshima.kubwa wala hakushangilia,dah soka bana.

Dah unajua show ya.kibabe ya kufungia wiki ilikuwa wapi....huko Santiago bernabeu,mashabiki elfu 85 walijazana,barca waliingia kwa unyonge,dah bila neymar maisha yangekuaje,lakini watu wakasahau kwamba kuna Mfalme mmoja tu ndani ya barca,king messi,akawapiga bao mbili za kibabe huku ubabe wa Ramos ukimpeleka nje kwa red card,dakika 90,barca 3 Madrid 2,,utamu wa la liga unazidi kunoga.

Kwa Leo tuishie hapa kwenye weekend yetu ya kibabe,ila.tumalizie kwa kuhoji,kamati ya katiba na sheria ya TFF kwani hamkujua Simba hawakukidhi vigezo vya kukata rufaa? Na zile gharama za kuwalipia nauli viongozi na mchezaji wa kagera na marefariii analipa nani?

Tukutane week ijayo.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top