Timu ya soka ya Simba ssc imepunguzwa kasi katika mbio za kutwaa ubingwa wa Ligi kuu Tanzania bara na Toto Africa ya mwanza baada ya kulazimishwa sare ya bila kufungana
Simba itabidi wajilaumu wenyewe kwakushindwa kuibuka na pointi tatu kwani walimiliki mpira kwa kiasi kikubwa na washambuliaji wake wangekua makini dakika 45 za kwanza wangekua wanaongoza goli mbili za wazi alizo kosa Fredrick Blagnon.
Kipindi cha Pili Toto walicheza kwa nidhamu yavkukaba na kushambulia kwakushtukiza kitendo ambacho kili wafanya Simba nao kuwa makini wakati wanashambulia.
Mpaka Mwamuzi anapuliza filimbi kuashiria mpira umekwisha Toto Africa bila na Simba bila
Mwamuzi Jacob Adongo alimzawadia kadi za njano wachezaji wa tatu watoto kwakucheza rafu mbaya Hussen Suleyman Jafari Salum na Hamim Abduli.
Kocha wa simba aliwatoa Mohamed Ibrahim, Shiza Kichuya na Loudiot Mavugo nafasi zao akawaingiza Mwinyi Kazimoto, Juma Luizio na Ibrahim Ajibu
Kwaupande wa toto walitoka Jamal Sud na nafasi yake akaingia Ahmad Mumba.
TOTO WAIPUNGUZA KASI SIMBA KIRUMBA
Title: TOTO WAIPUNGUZA KASI SIMBA KIRUMBA
Author: SDF SPORTS
Rating 5 of 5 Des:
Author: SDF SPORTS
Rating 5 of 5 Des:
Timu ya soka ya Simba ssc imepunguzwa kasi katika mbio za kutwaa ubingwa wa Ligi kuu Tanzania bara na Toto Africa ya mwanza baada ya kulaz...
Post a Comment