SDF SPORTS SDF SPORTS Author
Title: YANGA YATUPWA KWA WARABU KOMBE LA SHIRIKISHO
Author: SDF SPORTS
Rating 5 of 5 Des:
Mabingwa ligi kuu Vodacom Tanzania  Bara na wawakilishi pekee katika michuano ya kimataifa  Young Africa itamenyana na Mc Alger ya Algeri...
Mabingwa ligi kuu Vodacom Tanzania  Bara na wawakilishi pekee katika michuano ya kimataifa  Young Africa itamenyana na Mc Alger ya Algeria katika mchujo wa kuwania hatua ya makundi ya kombe la shirikisho Afrika.

Hii ni baada ya droo iliyofanyika mchana huu mjini Cairo Misri makao makuu ya shirikisho la soka Afrika (Caf).

Yanga imeangukia kombe la shirikisho baada ya kuondoshwa  katika michuano ya ligi ya mabingwa baada ya kupata sare ya bila kufungana na wenyeji Zanaco katika mchezo wa marejeano uliofanyika lusaka Zambia katika uwanja wa mashujaa.

mchezo wa awali Yanga akiwa mwenyeji alilazimishwa sare ya bao 1-1 na matokeo hayo Yanga ilijikuta ikiondoshwa katika michuano ya ligi mabingwa kwa mabao ya ugenini.


Yanga itaanza kucheza mchezo wake wa kwanza wa kombe la shirikisho Jijini Dar Es Salaam  kati ya April 7 hadi 9 na mchezo wa marejeano utapigwa April 14 hadi 19 nchini Algeria.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top