SDF SPORTS SDF SPORTS Author
Title: SIMBA YATOA DOZI KWA MTIBWA
Author: SDF SPORTS
Rating 5 of 5 Des:
Timu ya soka ya Simba sc imeendeleza wimbi la ushindi baada ya kuifunga timu ya Mtibwa Sugar kwa magoli 2-0 katika mchezo wa ligi kuu ya ...

Timu ya soka ya Simba sc imeendeleza wimbi la ushindi baada ya kuifunga timu ya Mtibwa Sugar kwa magoli 2-0 katika mchezo wa ligi kuu ya vodacom uliochezwa katika uwanja wa Uhuru leo hii.

Mpaka mapumziko matokeo yalikuwa 0-0, Kipindi cha pili kilianza kwa kasi sana huku timu ya Simba ikifanikiwa kupata goli la kwanza kupitia mshambuliaji wake Ibrahim Ajibu aliyeunganisha kwa kichwa kona iliyopiga na Shizya Kichuya katika dakika ya 52. 


Goli la pili la Simba lilifungwa na Laudit Mavugo kwa shuti kali sana baada ya kupokea pasi ya Mwinyi Kazimoto. Mpaka mwamuzi Raphael Adong'o kutoka mkoa wa Mara akipuliza kipinga cha mwisho matokeo yalikuwa wa goli 2-0.


About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top