
Uzinduzi huo umefanywa na Rais wa Simba, Evans Aveva ambaye aliwashukuru EAG ambao ni kampuni iliyoingia mkataba kwa ajili ya masuala ya masoko ya klabu hiyo ambao walibuni mradi huo.
Aveva alisema kuwa wataendelea kufungua maduka zaidi katika ya jiji na baadaye kwenye mikoa mbalimbali ya Tanzania ili mtu yeyote aweze kujipatia vifaa hivyo ambapo mapato yatakuwa yanaisadia klabu kwenye matumizi mbalimbali.
Nawashukuru EAG ambao
tuliingia nao mkataba mwaka jana, walianza na kazi ya jezi na leo hii
tunazindua duka linalouza vifaa mbalimbali ambavyo si jezi, duka lilingine
tutafungua Makao Makuu ya klabu na baaye sehemu zingine za jiji na nje ya
mji," alisema Aveva.
Kwa upande wa Mkurugenzi wa EAG, Imani Kajula alisema kuwa "Hivi vifaa pia vitakuwa vinatapatika kwa njia ya mtandao kama ilivyokuwa wakati wa uuzaji wa jezi zetu, kwani wadau wengi pia walinunua jezi kupitia mtandao,".
Kwa upande wa Mkurugenzi wa EAG, Imani Kajula alisema kuwa "Hivi vifaa pia vitakuwa vinatapatika kwa njia ya mtandao kama ilivyokuwa wakati wa uuzaji wa jezi zetu, kwani wadau wengi pia walinunua jezi kupitia mtandao,".
Post a Comment