Kalaghe Secondary School Kalaghe Secondary School Author
Title: GUARDOLA KUWA MENEJA MAN CITY
Author: Kalaghe Secondary School
Rating 5 of 5 Des:
Mhispania Pep Guardiola ametia saini mkataba wa miaka mitatu kuwa meneja mpya wa Manchester City baada ya msimu huu kumalizika. Guardiola...
Mhispania Pep Guardiola ametia saini mkataba wa miaka mitatu kuwa meneja mpya wa Manchester City baada ya msimu huu kumalizika.
Guardiola, atachukua majukumu hayo kuanzia Julai, klabu hiyo ya Ligi ya Premia imetangaza.
Manuel Pellegrini ataondoka klabu hiyo Juni 30 baada ya kumalizika kwa msimu wa sasa.
Katika taarifa yao City wamesema kuwa Pellegrin ameshirikishwa kwa kiwango kikubwa katika mchakato huo na kwamba kwa sasa ameweka nguvu zake katika kuhakikisha anamaliza msimu huu kwa mafanikio. 

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top