Kalaghe Secondary School Kalaghe Secondary School Author
Title: MAYANJA AWA KOCHAMSAIDIZI SIMBA
Author: Kalaghe Secondary School
Rating 5 of 5 Des:
Jackson Mayanja aliyekuwa akiifundisha Coastal Union ya jijini Tanga leo ametua Simba kuwa msaidizi wa Dylan Kerr ambaye hakupata msaid...

Jackson Mayanja aliyekuwa akiifundisha Coastal Union ya jijini Tanga leo ametua Simba kuwa msaidizi wa Dylan Kerr ambaye hakupata msaidizi tangu Seleman Matola ajiuzulu.

Mayanja ametua jana mchana na kuungana na kikosi cha Simba kilichopo visiwani Zanzibar ambako kinashiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi na leo watacheza mechi ya nusu fainali dhidi ya Mtibwa Sugar.


Mayanja amewahi kuifundisha Kagera Sugar kwa mafanikio makubwa na tangu aondoke timu hiyo imekuwa ikisuasua kwenye ligi hata Coastal Union haijafanya vizuri ingawa sababu kubwa ni za kiutawala.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top