Katika kuenzi mchango wa wachezaji wake wa Zamani wenye malengo ya kufundisha soka, imeamua kugharamia kozi ya ukocha daraja C kwa wachezaji wake wa Zamani watatu: Suleiman Matola ambaye pia ni kocha msaidizi wa Simba, George Lucas “Gaza” na Yusuf Macho “Musso”.
Akiongea wakati wa kukabithi hundi za malipo kwa wachezaji hao, Rais wa Simba Evans Aveva alisema ” wakati tunaingia madarakani tuliahidi kusaidia wachezaji wetu wa Zamani kujiendeleza hususani kwenye ukocha, hawa ni Watu muhimu mno kwa timu yetu na walitoa mchango mkubwa kwa timu yetu. Uongozi wangu utaendelea kutekeleza kwa vitendo ahadi za wakati wa uchaguzi”.


Post a Comment