SDF SPORTS SDF SPORTS Author
Title: KING KIKI KAKERE WAMLIZA HUSSEIN JUMBE
Author: SDF SPORTS
Rating 5 of 5 Des:
Mwanamuziki nguli wa muziki dansi nchini,Hussein juzi alijikuta akimwaga  machozi ya furaha wakati wa mazoezi ya pamoja na mastaa wenza...
Mwanamuziki nguli wa muziki dansi nchini,Hussein juzi alijikuta akimwaga 
machozi ya furaha wakati wa mazoezi ya pamoja na mastaa wenzake wanaounda 
kikosi cha timu ya Taifa dansi yaliyofanyika katika Ukumbi wa CCM Mwinjuma 
Mwananyamala jijini Dar es Salaam.

Tukio hilo lilitokea mara baada ya wanamuziki wenzake Kikumbi Mwanza 
Mpango na Juma Kakere kuingiza vipande vipya vya mashairi katika wimbo wa 
Jumbe 'Siri ya Nini' ambavyo vilimsisimua na kujikuta akilia kwa furaha.
"Kiki na Kakere wameniliza kwakweli sikutegemea kama wangeweza kunishtua 

kwa kiasi hiki kwa namna walivyoingiza hisia mpya kwenye wimbo huu na 
kuifanya Remix kunoga,nimelia kwa furaha kwakweli".

Alisema, walikuwa wakiufanyia mazoezi wimbo huo bila kupangilia kama 
wangeongeza kitu chochote lakini kwa namna kombinesheni ya watatu hao 
ilivyonoga atalazimika kuingia nao studio kuurekodi upya.

Mastaa hao dansi wako kambini wakijifua kujiandaa na mpambano dhidi ya 
bendi ya Msondo Ngoma utakaofanyika Sept.2 mwaka huu katika Ukumbi wa 

Travertine Magomeni jijini Dar es Salaam.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top