Mwamuzi wa kike wa Kimataifa wa Tanzania mwenye beji ya FIFA, Jonesia
Rukyaa ameteuliwa kuungana na waamuzi kutoka nchini Kenya kuchezesha
mchezo wa kuwania kufuzu kwa Fainali za Kombe la Dunia kwa Wanawake
wenye umri chini ya miaka 17 (WWC-Q 17) mwishoni mwa mwezi huu.
Jonesia Rukyaa atakua mwamuzi wa akiba katika mchezo huo kati ya
Misri dhidi ya Cameroon utakaochezwa jijini Cairo wikiendi ya tarehe
25,26,27 Machi, 2016.
Mwamuzi wa kati katika mchezo huo atakua ni Carolyne Wanjala (Kenya),
akisaidiwa na Carolyne Kiles (Kenya), Mary Njoroge (Kenya), huku
kamisaa wa mchezo huo akiwa ni Leah Annette Dabanga kutoka nchi ya
Afrika ya Kati.
Home
»
Kitaifa
» ALIECHEZESHA SIMBA NA YANGA KUCHEZESHA MCHEZO WA KUFUZU KOMBE LA DUNIA KWA WANAWAKE CAIRO
About Author

Advertisement

Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment